Machapisho

JE KAMA UKIUTAFUTA KWANZA UFALME WA MUNGU UTAPATA NINI?

Picha
Hello habari ndugu? Karibu tena siku ya Leo tena tunapoendelea kujifunza zaidi kuhusu neno la Mungu pamoja na mbinu mbalimbali za mafanikio, ujasiriamali na biashara. Leo nitazungumzia suala la maisha yetu ya kawaida kabisa. Watu wengi tumekuwa tukihangaikia maisha ambalo ni jambo zuri sana kwa sababu ndipo tunapopapata ridhiki yetu ya kila Siku. Lakini leo ndugu nataka turudi kwenye maandiko matakatifu yaani biblia kuhusu suala la utafutaji na je inatuhasa tutafute kitu gani kwanza ili tuweze kupata mafanikio Yetu ya kimwili Na kiroho pia. Naomba usome na mimi kwenye biblia katika kitabu cha MATHAYO 6:33-34 kama ifuatavyo; 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Kwa hiyo rafiki yangu nakushauri sana jitahidi kutafuta ufalme wa Mungu kwanza kabla ya kitu chochote hapa duniani na hapo ndipo Mungu atakubariki hata kazi ya mikono yako. Una...

MADHARA UTAKAYOPATA KAMA USIPOTUMIA KIPAJI CHAKO

Picha
Leo napenda nizungumze na wewe rafiki yangu juu ya talanta au kipaji chako ulichopewa na Mungu . Yawezekana rafiki yangu wewe una kipaji cha uimbaji au uchoraji  au uandishi au uigizaji  n.k.  Pia labda wewe umepewa kipaji au Huduma Fulani ambayo unatakiwa kumtumikia Mungu kupitia hicho kipaji au Huduma uliyopewa Mungu. Lakini yawezekana haujatumia kipaji au talanta kutokana sababu au visingizio mbali mbali kama kutokujiamini , kujisikia , maringo, ulegevu, uvivu au unataka hadi ubembelezwe na sababu zingine kadhalika Naomba usome biblia  na mimi katika kitabu cha MATHAYO 25: 14-30. Hii imelezea watumishi watatu walioachiwa talanta na bwana wao. Mmoja alipewa talanta kumi, mwingine  talanta tano na mwingine talanta moja. Aliyepewa talanta kumi alienda akafanya biashara akapata talanta kumi nyingine vivyo hivyo aliyepewa talanta tano akazalisha talanta tano zingine baada ya kufanya biashara. Lakini aliyepewa talanta moja akachimba shimo akaifukia talanta yake ...

JE NI SAUMU IPI INAKUBALIKA MBELE ZA MUNGU?

Picha
JE UMESHAWAHI  KUJIULIZA NI KWA NINI TUNAFUNGA NA KUOMBA? NA JE NI SAUMU IPI INAYOKUBALIKA MBELE ZA MUNGU? WATU WENGI TUMEKUWA TUKIFUNGA NA KUOMBA LAKINI HATUPATI MAJIBU YA MAOMBI  YETU KAMA WALIVYOKUWA WANA WA ISRAELI KATIKA KITABU CHA ISAYA 58:3-5 LAKINI UKISOMA KATIKA ISAYA 58:6-7 INAELEZA MAMBO 8 YA KUZINGATIA ILI SAUMU YETU IKUBALIKE MBELE ZA MUNGU NAYO NI 1. KUFUNGUA VIFUNGO VYA UOVU 2. KUZILEGEZA KAMBA ZA NIRA. 3. KUWAACHIA  HURU WALIONEA 4. KUVUNJA KILA NIRA. 5. KUWAGAWIA WENYE NJAA CHAKULA CHAKO. 6. KUWALETA MASKINI WALIOTUPWA NJE NYUMBANI KWAKO. 7. UMWONAPO  MTU ALIYE UCHI, UMVIKE NGUO 8. WALA USIJIFICHE NA MTU MWENYE DAMU MOJA NAWE. BASI  NDUGU TUZINGATIE MAMBO HAYA ILI MAOMBI NA SAUMU ZETU IKUBALIKE  MBELE ZA BWANA. Wako katika ujenzi wa Taifa Mwalimu Caleb Samuel Bandora. BONYEZA MAANDISHI HAYA ILI UJIUNGE NAMI NIWE NAKUTUMIA MAKALA NZURI NA MASOMO YA NENO LA MUNGU , UJASIRIAMALI, BIASHARA NA MAFANIKIO KWA NJIA YA E...

FURAHA YA BWANA NDIYO NGUVU YANGU

Picha
BWANA YESU ASIFIWE MTUMISHI WA MUNGU. BIBLIA INASEMA KATIKA WAFILIPI 4:4-6 FURAHINI KATIKA BWANA TENA NASEMA FURAHINI. UPOLE WENU NA UJULIKANE NA WATU WOTE. MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE  BALI KATIKA KILA NENO KWA KUSALI NA KUOMBA PAMOJA NA KUSHUKURU, HAJA ZENU NA ZIJULIKANE NA MUNGU. MTUMISHI NAKUOMBEA MUNGU AKUPE KICHEKO KATIKA HUDUMA ULIYONAYO, FAMILIA YAKO, BIASHARA NA KAZI YAKO PIA BILA KUJALISHA UNAPITIA HALI GANI HAKIKA UKIMTEGEMEA YESU ATAKUSAIDIA KUSHINDA MAJARIBU UNAYOPITIA SASA. KAMA UNAHITAJI USHAURI, MAOMBI & MAOMBEZI TAFADHALI USISITE KUWASILIANA NAMI Wako katika ujenzi wa Taifa Mwalimu Caleb Samuel Bandora BONYEZA HAYA MAANDISHI ILI KUJIUNGA NAMI NIWE NAKUTUMIA MAKALA NZURI NA MASOMO YA NENO LA MUNGU, UJASIRIAMALI, BIASHARA NA MAFANIKIO KWA NJIA YA EMAIL KILA WIKI

Wanawake wa leo mnaweza kama alivyoweza esta

Picha
Wanawake wa leo mnaweza kama alivyoweza esta kubadilisha mawazo ya mfalme na akaokoa taifa la israeli lisiangamizwe basi nanyi pia mnaweza . Cha msingi mzidi kujiamini na kuthubutu kuchukua hatua zitazowaletea maendeleo. Ila msije mkamsahau Mungu maana yeye ndio kimbilio na msaada , bali  dumuni katika imani , kusali na kuomba ili Mungu azidi kuwabariki katika maisha yenu na mkawe mfano bora katika jamii. Nawaombea Mungu awabariki na azidi kuwasogeza kutoka hatua moja ya maisha hadi nyingine. Happy women's day to all women.